Sunday, 4 January 2015

Yanga yamtosa Kaseja CAF

Yanga yamtosa Kaseja CAF

Yanga imetuma CAF majina ya wachezaji 23 watakaoshiriki katika michuano ya kombe la shirikisho Afrika huku jina la mkongwe kipa Juma Kaseja likikosekana

KLABU ya Yanga imetuma CAF majina ya wachezaji 23 watakaoshiriki katika michuano ya kombe la shirikisho Afrika huku jina la mkongwe kipa Juma Kaseja likikosekana.

Kaseja aliyekosa namba kwenye kikosi cha Yanga tangu alipojiunga nayo kwenye dirisha dogo msimu uliopita hajahudhuria kwenye mazoezi ya timu hiyo tangu ilipoanza maandalizi ya mechi za raundi ya nane kwa sababu ya kutocheza kwenye kikosi cha kwanza.

Afisa mawasiliano wa klabu ya Yanga Jery Muro, ameiambia Goal kuwa wameliondoa jina la Kaseja kwasababu ameshindwa kufanya mazoezi na wenzake kwa kipindi cha mwezi mmoja bila sababu maalumu huku akiendelea kulipwa mshahara kama kawaida.

Yanga imepangwa kuanza na klabu ya BDF kutoka Botswana ambayo ni timu inayomilikiwa na jeshi la ulinzi la nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment